MOJA ya hulka ya mwanadamu ni kutopenda amani na utulivu uliovuka
mipaka. Hulka hii mwanadamu huianza tokea akiwa mtoto ndiyo maana
unaweza kuona mtoto anahangaika mgongoni huku akiwa yuko kwenye
mebeleko ya mama yake.
Si kwamba mtoto anahangaika kwa
vile ana hofu ya kuanguka kutoka kwenye mgongo wa aliyembebea, la
hasha, bali huwa amechoka na amani iliyopitiliza.
Akiwa
mgongoni pale anakuwa yuko salama, ana kinga kamili kutoka kwa amtu
aliyembeba, lakini bado hakubali atanyoosha mikono, atatoa miguu na
kujirusha kama vile hafurahii kitendo cha kubebwa.
Mtoto
anapokuwa katika mazingira haya sio kwamba hafurahii kubebwa wala si
kuwa anatimiza ule msemo usemao "abebwaye hujikaza", hapana, bali
hufanya hivyo katika kudhihirisha tu ile hulka ya mwanadamu kuwa
huchoshwa hata na amani.
Ziko hata nchi ambazo huchokonoa
hiki na kile na hatimaye kusababisha machafuko wakati kulikuwa na amani
ya kutosha na kulikuwa hakuna hoja ya msingi ya kuwepo madai yoyote
yale.
Hata kwenye uwanja wa mapenzi hali haiko tofauti.
Ndiyo maana unaweza ukawaona watu wanaachana huku watu wengine
wakishangaa kwa vile walikuwa wanawaona wana mapenzi mazito.
Hali
hiyo inatokana na watu hao kuchoshwa na amani, kwa hiyo wanatafuta kila
njia ili uwepo mgongano kati yao.
Bendi maarufu ya muziki
wa dansi ya DDC Mlimani Park inayopiga mtindo wa Sikinde iliwahi kutoa
wimbo mmoja ambao ulikuwa unazungumza juu ya wanandoa wanapogombana.
Katika
wimbo huo inaelezwa kuwa mwanaume anakuwa mkorofi na anapokosana na
mkewe na kurudi kwao anakwenda kutafuta suluhu.
Sikinde
wanaeleza kwamba mwanaume huyo ambaye walimpa jina la "Chuma ulete"
akiambiwa aangukie anatoa fedha nyingi kuliko mahari aliyotoa.
Ni
ukweli usiobishika kwamba wako watu wa namna hii ambao wakigombana na
wapenzi wao hulazimishwa kuangukia. Wako wanaotoa fedha, nguo, ng'ombe,
mbuzi na vinywaji.
Hawa akina chuma ulete huwezi
kuwalaumu hata kidogo kwani ndiyo hulka ya mwanadamu au ndio msingi wa
maisha kuwa hakuwezi kuwa na utulivu na amani kupita kiasi.
Ndiyo
maana hata maji kwenye mtungi hubumburika bila hata ya kuguswa na mtu
au vyombo kwenye kabati hugongana bila ya kuwepo kwa mkono wa mtu.
Pamoja
na kwamba ni vigumu kuwa na mapenzi yasiyoingiwa na migogoro hata
kidogo; vinginevyo labda muwe munadanganyana kama wacheza sinema hivi,
ni vizuri kujaribu kuipunguza kwa kadri inavyowezekana.
Lakini
jambo la msingi zaidi inapotokea mgongano kati ya wapenzi ni
kuhakikisha kwamba msiwe miamba wote wawili. Kila mmoja asijifanye
kifaru na kutaka kuoneshana umwamba na mwenzake, hapo hamutafanikiwa na
mapenzi yenu yanaweza kukatika huku munapendana.
Unapotokea
ugomvi baina ya wapenzi si kwamba hawapendani tena au kuna mmoja
kapata mwingine au anamchukia mwenzake, la hasha ni hali ileile tu ya
kuwepo mikwaruzano ili maisha yawepo.
Kwa hiyo
kinachotakiwa kutokea iwapo mgongano unazuka baina ya wawili wapendanao
ni kwa mmoja kuwahi kuomba radhi na mwingine kuikubali hiyo rahi
aliyoombwa bila ya kuweka masharti yoyote ya |